6. Sauti ya fujo itokayo mjini!Sauti itokayo hekaluni!Sauti ya BWANA awalipaye adui zake adhabu!
7. Kabla hajaona utungu alizaa;Kabla maumivu yake hayajampata,Alizaa mtoto mwanamume.
8. Ni nani aliyesikia neno kama hili?Ni nani aliyeona mambo kama haya?Je! Nchi yaweza kuzaliwa siku moja?Taifa laweza kuzaliwa mara?Maana Sayuni, mara alipoona utungu,Alizaa watoto wake.
9. Je! Mimi nilete wana karibu na kuzaliwa, nisizalishe? Asema BWANA; mimi nizalishaye, je! Nilifunge tumbo? Asema Mungu wako.