3. Nalikanyaga shinikizoni peke yangu;Wala katika watu hakuwapo mtu pamoja nami;Naam, naliwakanyaga kwa hasira yangu,Naliwaponda kwa ghadhabu yangu;Na mavazi yangu yametiwa madoa kwa damu yao,Nami nimezichafua nguo zangu zote.
4. Maana siku ya kisasi ilikuwamo moyoni mwangu,Na mwaka wao niliowakomboa umewadia.
5. Nikatazama, wala hakuna wa kusaidia;Nikashangaa kwa kuwa hakuna mwenye kutegemeza;Basi, mkono wangu mwenyewe uliniletea wokovu,Ghadhabu yangu ndiyo iliyonitegemeza.
6. Nikazikanyaga kabila za watu kwa hasira yangu,Nikawalevya kwa ghadhabu yangu,Nami nikaimwaga damu yao chini.