8. Ni nani hawa warukao kama wingu,Na kama njiwa waendao madirishani kwao?
9. Hakika yake visiwa vitaningojea,Na merikebu za Tarshishi kwanza,Ili kuleta wana wako kutoka mbali,Na fedha yao na dhahabu yao pamoja nao,Kwa ajili ya jina la BWANA, Mungu wako,Kwa ajili yake Mtakatifu wa Israeli,Kwa kuwa amekutukuza wewe.
10. Na wageni watajenga kuta zako,Na wafalme wao watakuhudumu;Maana katika ghadhabu yangu nalikupiga,Lakini katika upendeleo wangu nimekurehemu.
11. Malango yako nayo yatakuwa wazi daima;Hayatafungwa mchana wala usiku;Ili watu wapate kukuletea utajiri wa mataifa,Na wafalme wao wakiongozwa pamoja nao.