20. Jua lako halitashuka tena,Wala mwezi wako hautajitenga;Kwa kuwa BWANA mwenyewe atakuwa nuru yako ya milele;Na siku za kuomboleza kwako zitakoma.
21. Watu wako nao watakuwa wenye haki wote,Nao watairithi nchi milele;Chipukizi nililolipanda mimi mwenyewe,Kazi ya mikono yangu mwenyewe,Ili mimi nitukuzwe.
22. Mdogo atakuwa elfu,Na mnyonge atakuwa taifa hodari;Mimi, BWANA, nitayahimiza hayo wakati wake.