Isa. 60:1-4 Swahili Union Version (SUV)

1. Ondoka, uangaze; kwa kuwa nuru yako imekuja,Na utukufu wa BWANA umekuzukia.

2. Maana, tazama, giza litaifunika dunia,Na giza kuu litazifunika kabila za watu;Bali BWANA atakuzukia wewe,Na utukufu wake utaonekana juu yako.

3. Na mataifa wataijilia nuru yako,Na wafalme kuujia mwanga wa kuzuka kwako.

4. Inua macho yako, utazame pande zote;Wote wanakusanyana; wanakujia wewe;Wana wako watakuja kutoka mbali.Na binti zako watabebwa nyongani.

Isa. 60