11. Nami nitafanya milima yangu yote kuwa njia, na njia kuu zangu zitatukuzwa zote.
12. Tazama, hawa watakuja kutoka mbali; na tazama, hawa kutoka kaskazini, na kutoka magharibi, na hawa kutoka nchi ya Sinimu.
13. Imbeni, enyi mbingu; ufurahi, Ee nchi;Pazeni sauti ya kuimba, enyi milima;Kwa kuwa BWANA amewafariji watu wake,Naye atawahurumia watu wake walioteswa.
14. Bali Sayuni alisema, YEHOVA ameniacha, Bwana amenisahau.