Isa. 49:11-14 Swahili Union Version (SUV)

11. Nami nitafanya milima yangu yote kuwa njia, na njia kuu zangu zitatukuzwa zote.

12. Tazama, hawa watakuja kutoka mbali; na tazama, hawa kutoka kaskazini, na kutoka magharibi, na hawa kutoka nchi ya Sinimu.

13. Imbeni, enyi mbingu; ufurahi, Ee nchi;Pazeni sauti ya kuimba, enyi milima;Kwa kuwa BWANA amewafariji watu wake,Naye atawahurumia watu wake walioteswa.

14. Bali Sayuni alisema, YEHOVA ameniacha, Bwana amenisahau.

Isa. 49