Isa. 42:18-20 Swahili Union Version (SUV)

18. Sikilizeni, enyi viziwi; tazameni, enyi vipofu, mpate kuona.

19. Ni nani aliye kipofu, ila mtumishi wangu? Au aliye kiziwi, kama mjumbe wangu nimtumaye? Ni nani aliye kipofu, kama yeye aliye na amani? Naam, kipofu kama mtumishi wa BWANA?

20. Unaona mambo mengi, lakini huyatii moyoni; masikio yake ya wazi, lakini hasikii.

Isa. 42