13. Nawe ulisema moyoni mwako, Nitapanda mpaka mbinguni,Nitakiinua kiti changu juu kuliko nyota za Mungu;Nami nitaketi juu ya mlima wa mkutano,Katika pande za mwisho za kaskazini.
14. Nitapaa kupita vimo vya mawingu,Nitafanana na yeye Aliye juu.
15. Lakini utashushwa mpaka kuzimu;Mpaka pande za mwisho za shimo.
16. Wao wakuonao watakukazia macho,Watakuangalia sana, wakisema,Je! Huyu ndiye aliyeitetemesha dunia,Huyu ndiye aliyetikisa falme;