5. Mbele zake ilikwenda tauni,Na makaa ya moto yakatoka miguuni pake.
6. Akasimama, akaitetemesha dunia;Akatazama, akawasitusha mataifa;Na milima ya zamani ikatawanyika;Vilima vya kale vikainama;Miendo yake ilikuwa kama siku za kale.
7. Naliziona hema za Kushani katika taabu;Mapazia ya nchi ya Midiani yakatetemeka.
8. Je! BWANA aliikasirikia mito?Je! Hasira yako ilikuwa juu ya mito,Au ghadhabu yako juu ya bahari,Hata ukapanda farasi zako,Katika magari yako ya wokovu?
9. Uta wako ukafanywa wazi kabisa;Viapo walivyopewa kabila vilikuwa neno thabiti;Ukaipasua nchi kwa mito.
10. Milima ilikuona, ikaogopa;Gharika ya maji ikapita;Vilindi vikatoa sauti yake,Vikainua juu mikono yake.
11. Jua na mwezi vikasimama makaoni mwao;Mbele ya nuru ya mishale yako ilipotapakaa,Mbele ya mwangaza wa mkuki wako umeremetao.
12. Ulikwenda katikati ya nchi kwa ghadhabu;Ukawapura mataifa kwa hasira.