6. Mtu asiwadanganye kwa maneno yasiyo na maana; kwa kuwa kwa sababu ya hayo hasira ya Mungu huwajia wana wa uasi.
7. Basi msishirikiane nao.
8. Kwa maana zamani ninyi mlikuwa giza, bali sasa mmekuwa nuru katika Bwana; enendeni kama watoto wa nuru,
9. kwa kuwa tunda la nuru ni katika wema wote na haki na kweli;
10. mkihakiki ni nini impendezayo Bwana.
11. Wala msishirikiane na matendo yasiyozaa ya giza, bali myakemee;