Efe. 4:1-4 Swahili Union Version (SUV)

1. Kwa hiyo nawasihi, mimi niliye mfungwa katika Bwana, mwenende kama inavyoustahili wito wenu mlioitiwa;

2. kwa unyenyekevu wote na upole, kwa uvumilivu, mkichukuliana katika upendo;

3. na kujitahidi kuuhifadhi umoja wa Roho katika kifungo cha amani.

4. Mwili mmoja, na Roho mmoja, kama na mlivyoitwa katika tumaini moja la wito wenu.

Efe. 4