1. Kwa hiyo nawasihi, mimi niliye mfungwa katika Bwana, mwenende kama inavyoustahili wito wenu mlioitiwa;
2. kwa unyenyekevu wote na upole, kwa uvumilivu, mkichukuliana katika upendo;
3. na kujitahidi kuuhifadhi umoja wa Roho katika kifungo cha amani.
4. Mwili mmoja, na Roho mmoja, kama na mlivyoitwa katika tumaini moja la wito wenu.