18. Misafara isafiriyo kwa njia yao hugeuka;Hukwea kwenda barani, na kupotea.
19. Misafara ya Tema huvitazama,Majeshi ya Sheba huvingojea.
20. Wametahayari kwa sababu walitumaini;Wakaja huku, nao walifadhaika.
21. Kwani sasa ninyi mmekuwa vivyo;Mwaona jambo la kutisha, mkaogopa.
22. Je! Nilisema, Nipeni?Au, Nitoleeni toleo katika mali yenu?
23. Au, Niokoeni na mkono wa adui?Au, Nikomboeni na mikono ya hao waoneao?