5. Mavuno yake wale wenye njaa huyala,Na kuyatwaa hata kuyatoa miibani,Nao wenye kiu huzitwetea mali zao.
6. Kwani taabu haitoki mchangani,Wala mashaka hayachipuki katika nchi;
7. Lakini mwanadamu huzaliwa ili apate mashaka,Kama cheche za moto zirukavyo juu.
8. Lakini mimi ningemtafuta Mungu,Ningemwekea Mungu daawa yangu;