Ayu. 5:19-22 Swahili Union Version (SUV)

19. Yeye atakuokoa na mateso sita;Naam, hata katika saba hapana uovu utakaokugusa.

20. Wakati wa njaa atakukomboa na mauti;Na vitani atakukomboa na nguvu za upanga.

21. Utafichwa na mapigo ya ulimi;Wala usiogope maangamizo yatakapokuja.

22. Wewe utayacheka maangamizo na njaa;Wala hutawaogopa wanyama wakali wa nchi.

Ayu. 5