19. Yeye atakuokoa na mateso sita;Naam, hata katika saba hapana uovu utakaokugusa.
20. Wakati wa njaa atakukomboa na mauti;Na vitani atakukomboa na nguvu za upanga.
21. Utafichwa na mapigo ya ulimi;Wala usiogope maangamizo yatakapokuja.
22. Wewe utayacheka maangamizo na njaa;Wala hutawaogopa wanyama wakali wa nchi.