Ayu. 5:16-21 Swahili Union Version (SUV)

16. Basi hivi huyo maskini ana matumaini,Na uovu hufumba kinywa chake.

17. Tazama, yu heri mtu yule Mungu amwadhibuye;Kwa hiyo usidharau kurudiwa na huyo Mwenyezi.

18. Kwani yeye huumiza, lakini tena huuguza;Yeye hutia jeraha, na mikono yake huponya.

19. Yeye atakuokoa na mateso sita;Naam, hata katika saba hapana uovu utakaokugusa.

20. Wakati wa njaa atakukomboa na mauti;Na vitani atakukomboa na nguvu za upanga.

21. Utafichwa na mapigo ya ulimi;Wala usiogope maangamizo yatakapokuja.

Ayu. 5