21. Pumzi zake huwasha makaa,Na miali ya moto hutoka kinywani mwake.
22. Katika shingo yake hukaa nguvu,Na utisho hucheza mbele yake.
23. Manofu ya nyama yake hushikamana;Yanakazana juu yake; hayawezi kuondolewa.
24. Moyo wake una imara kama jiwe;Naam, imara kama jiwe la chini la kusagia.
25. Anapojiinua, mashujaa huogopa;Kwa sababu ya woga wao huvunjwa moyo.