Ayu. 41:21-25 Swahili Union Version (SUV)

21. Pumzi zake huwasha makaa,Na miali ya moto hutoka kinywani mwake.

22. Katika shingo yake hukaa nguvu,Na utisho hucheza mbele yake.

23. Manofu ya nyama yake hushikamana;Yanakazana juu yake; hayawezi kuondolewa.

24. Moyo wake una imara kama jiwe;Naam, imara kama jiwe la chini la kusagia.

25. Anapojiinua, mashujaa huogopa;Kwa sababu ya woga wao huvunjwa moyo.

Ayu. 41