17. Yeye hutikisa mkia wake mfano wa mwerezi;Mishipa ya mapaja yake yanaungamana pamoja.
18. Mifupa yake ni kama mirija ya shaba;Mbavu zake ni kama vipande vya chuma.
19. Yeye ni mkuu wa njia za Mungu;Yeye aliyemfanya alimpa upanga wake.
20. Hakika milima humtolea chakula;Hapo wachezapo wanyama wote wa barani.
21. Hulala chini ya miti yenye vivuli,Mafichoni penye mianzi, na matopeni.