Ayu. 40:17-21 Swahili Union Version (SUV)

17. Yeye hutikisa mkia wake mfano wa mwerezi;Mishipa ya mapaja yake yanaungamana pamoja.

18. Mifupa yake ni kama mirija ya shaba;Mbavu zake ni kama vipande vya chuma.

19. Yeye ni mkuu wa njia za Mungu;Yeye aliyemfanya alimpa upanga wake.

20. Hakika milima humtolea chakula;Hapo wachezapo wanyama wote wa barani.

21. Hulala chini ya miti yenye vivuli,Mafichoni penye mianzi, na matopeni.

Ayu. 40