10. Haya! Jivike sasa fahari na ukuu;Jipambe heshima na enzi.
11. Mwaga mafuriko ya hasira zako,Ukamtazame kila mtu mwenye kiburi, ukamdhili.
12. Mtazame kila mtu mwenye kiburi ukamshushe,Ukawakanyage waovu hapo wasimamapo.
13. Wafiche mavumbini pamoja,Wafunge nyuso zao mahali palipositirika.