1. Moyo wangu hunitetema kwayo pia,Nao hutoka mahali pake.
2. Zisikizeni hizo kelele za sauti yake,Na uvumi utokao kinywani mwake.
3. Yeye huituma iende chini ya mbingu zote,Na radi yake hata miisho ya nchi.
4. Baadaye sauti hunguruma;Yeye hunguruma kwa sauti ya ukuu wake;Hazizuii hapo sauti yake isikiwapo.