15. Yeye humponya aliyetaabika kwa njia ya taabu yake,Na kuyafunua masikio yao kwa maonevu.
16. Naam, yeye angekuongoza utoke katika msibaHata mahali penye nafasi, ambapo hapana msonge;Na kilichowekwa mezani pako kingejaa mafuta.
17. Lakini umejaa hukumu ya waovu;Hukumu na haki hukushika.
18. Basi ujitunze, isije hasira ikakuvuta hata ukafanya mzaha;Wala usikubali ukuu wa ukombozi ukugeuze.
19. Je! Mali yako yatatosha, hata usiwe katika taabu,Au uwezo wote wa nguvu zako?
20. Usiutamani usiku,Wakati watu wakatwapo katika mahali pao.