24. Yeye huwavunja-vunja mashujaa pasina kuwachunguza,Na kuwaweka wengine mahali pao.
25. Kwa sababu hiyo yeye huyatafiti matendo yao;Naye huwapindia usiku, wakaangamia.
26. Yeye huwapiga kama watu wabayaWaziwazi mbele ya macho ya wengine;
27. Kwa sababu walikengeuka, wasimwandame yeye,Wasikubali kuzishika njia zake hata moja;
28. Hata wakafanya kilio cha maskini kumfikilia,Naye akasikia kilio cha hao wateswao.