Ayu. 34:24-28 Swahili Union Version (SUV)

24. Yeye huwavunja-vunja mashujaa pasina kuwachunguza,Na kuwaweka wengine mahali pao.

25. Kwa sababu hiyo yeye huyatafiti matendo yao;Naye huwapindia usiku, wakaangamia.

26. Yeye huwapiga kama watu wabayaWaziwazi mbele ya macho ya wengine;

27. Kwa sababu walikengeuka, wasimwandame yeye,Wasikubali kuzishika njia zake hata moja;

28. Hata wakafanya kilio cha maskini kumfikilia,Naye akasikia kilio cha hao wateswao.

Ayu. 34