9. Sio wakuu walio wenye akili,Wala sio wazee watambuao hukumu.
10. Basi nilisema, Nisikilizeni mimi;Mimi nami nitawaonyesha nionavyo.
11. Tazama, niliyangojea maneno yenu,Nilizisikiliza nisikie hoja zenu,Hapo mlipokitafuta mtakalonena.
12. Naam, niliwasikiza ninyi,Na tazama, hapana mmoja aliyemshinda Ayubu,Wala kumjibu maneno yake, kati yenu.