Ayu. 32:9-12 Swahili Union Version (SUV)

9. Sio wakuu walio wenye akili,Wala sio wazee watambuao hukumu.

10. Basi nilisema, Nisikilizeni mimi;Mimi nami nitawaonyesha nionavyo.

11. Tazama, niliyangojea maneno yenu,Nilizisikiliza nisikie hoja zenu,Hapo mlipokitafuta mtakalonena.

12. Naam, niliwasikiza ninyi,Na tazama, hapana mmoja aliyemshinda Ayubu,Wala kumjibu maneno yake, kati yenu.

Ayu. 32