13. Waiharibu njia yangu,Wauzidisha msiba wangu,Watu wasio na msaidizi.
14. Wanijilia kama wapitao katika ufa mpana;Katikati ya magofu wanishambulia.
15. Vitisho vimenigeukia;Huifukuza heshima yangu kama upepo;Na kufanikiwa kwangu kumepita kama wingu.
16. Sasa nafsi yangu inamwagika ndani yangu;Siku za mateso zimenishika.
17. Wakati wa usiku mifupa yangu huchomeka ndani yangu,Na maumivu yanayonitafuna hayapumziki.