Ayu. 3:13-17 Swahili Union Version (SUV)

13. Maana hapo ningelala na kutulia;Ningelala usingizi; na kupata kupumzika;

14. Pamoja na wafalme na washauri wa dunia,Hao waliojijengea maganjoni;

15. Au pamoja na wakuu wenye dhahabu,Waliozijaza fedha nyumba zao;

16. Au, kama kuzikwa mimba iliyoharibika, nisingekuwako;Kama wachanga wasiouona mwanga kabisa.

17. Huko waovu huacha kusumbua;Huko nako hao waliochoka wapumzika

Ayu. 3