Ayu. 28:7-12 Swahili Union Version (SUV)

7. Njia ile hapana ndege mkali aijuaye,Wala jicho la tai halijaiona;

8. Wanyama wakali wajivunao hawajaikanyaga,Wala simba mkali hajaipita.

9. Huunyoshea mwamba wa gumegume mkono wake;Huipindua milima hata misingi yake.

10. Hukata mifereji kati ya majabali;Na jicho lake huona kila kito cha thamani

11. Hufunga vijito visichuruzike;Na kitu kilichostirika hukifunua.

12. Bali hekima itapatikana wapi?Na mahali pa ufahamu ni wapi?

Ayu. 28