Ayu. 27:19-23 Swahili Union Version (SUV)

19. Yeye hujilaza hali ni tajiri, lakini ndio mwisho;Hufunua macho yake, naye hayuko.

20. Vitisho vyampata kama maji mengi;Dhoruba humwiba usiku.

21. Upepo wa mashariki humchukua, naye huondoka;Na kumkumba atoke mahali pake.

22. Kwani Mungu atamtupia asimhurumie;Angependa kuukimbia mkono wake.

23. Watu watampigia makofi,Na kumzomea atoke mahali pake.

Ayu. 27