5. Hao waliokufa watetemaChini ya maji na hao wayakaao.
6. Kaburi li wazi mbele yake,Uharibifu nao hauna kifuniko.
7. Yeye hutandaza kaskazi juu ya nafasi isiyo na kitu,Na kuutundika ulimwengu pasipo kitu.
8. Huyafunga maji ndani ya mawingu yake mazito;Na hilo wingu halipasuki chini yake.
9. Husitiri uso wa kiti chake cha enzi,Na kulitandaza wingu lake juu yake.