8. Lakini huyo shujaa, nchi ilikuwa yake;Na huyo mwenye kusifiwa, yeye aliikaa.
9. Umewafukuza wanawake wajane hali ya utupu,Na mikono ya mayatima imevunjwa.
10. Kwa hiyo umezungukwa na mitego,Na hofu ya ghafula yakutaabisha,
11. Au je! Huoni giza,Na maji mengi yanayokufunika?
12. Je! Mungu hayuko mbinguni juu?Tena tazama umbali wa nyota, jinsi zilivyo juu!