18. Hata watoto wadogo hunidharau;Nikiondoka, huninena.
19. Wasiri wangu wote wanichukia;Na hao niliowapenda wamenigeukia.
20. Mfupa wangu unagandamana na ngozi yangu na nyama yangu,Nami nimeokoka na ngozi ya meno yangu tu.
21. Nihurumieni, nihurumieni, enyi rafiki zangu,Kwa maana mkono wa Mungu umenigusa.