4. Wewe ujiraruaye mwenyewe katika hasira yako,Je! Dunia itaachwa kwa ajili yako wewe?Au jabali litaondolewa mahali pake?
5. Naam, mwanga wa waovu utazimika,Wala mwali wa moto wake hautang’aa.
6. Mwanga hemani mwake utakuwa giza,Nayo taa iliyo juu yake itazimishwa.
7. Hatua zake za nguvu zitasongwa,Na shauri lake mwenyewe litamwangusha chini.