Ayu. 17:9-16 Swahili Union Version (SUV)

9. Lakini mwenye haki ataishika njia yake,Naye mwenye mikono safi atazidi kupata nguvu.

10. Lakini rudini; ninyi nyote, njoni sasa;Wala sitampata mtu mwenye hekima kati yenu.

11. Siku zangu zimepita, makusudi yangu yamevunjika,Hata hayo niliyo nayo moyoni mwangu.

12. Wabadili usiku kuwa mchana;Wasema, Mwanga u karibu kwa sababu ya giza.

13. Nikitazamia kuzimu kuwa nyumba yangu;Nikitandika malazi yangu gizani;

14. Ikiwa nimeuita uharibifu, Wewe u baba yangu;Na kuliambia buu, Wewe u mama yangu, na umbu langu;

15. Basi, tumaini langu li wapi?Na tumaini langu, ni nani atakayeliona?

16. Litashuka kwenye makomeo ya kuzimu,Itakapokuwapo raha mavumbini.

Ayu. 17