Ayu. 15:21-28 Swahili Union Version (SUV)

21. Sauti za utisho zi masikioni mwake;Katika kufanikiwa kwake mtekaji nyara atamjia juu yake;

22. Yeye hasadiki kwamba atarudi kutoka gizani,Naye hungojewa na upanga;

23. Hutanga-tanga ili apate chakula, akisema, Ki wapi?Ajua kwamba siku ya giza i tayari karibu yake;

24. Mateso na dhiki humtia hofu;Humshinda kama vile mfalme aliye tayari kwa vita;

25. Kwa kuwa amenyosha mkono wake juu ya Mungu,Na kuendelea kwa kiburi kinyume cha Mwenyezi;

26. Humshambulia na shingo ngumu,Kwa mafundo makubwa ya ngao zake;

27. Kwa kuwa amefunika uso wake na kunona kwake,Na kuwandisha mafuta kiunoni mwake;Naye amekaa katika miji iliyo ukiwa,

28. Katika nyumba ambazo hapana mtu azikaaye,Zilizokuwa tayari kuwa magofu.

Ayu. 15