6. Hema za wapokonyi hufanikiwa,Na hao wamkasirishao Mungu hukaa salama;Mikononi mwao Mungu huleta vitu vingi.
7. Lakini sasa waulize hao wanyama, nao watakufundisha;Na nyuni wa angani, nao watakuambia;
8. Au nena na nchi, nayo itakufundisha;Nao samaki wa baharini watakutangazia.