6. Hata ukauliza-uliza habari za uovu wangu,Na kuitafuta dhambi yangu,
7. Ujapojua ya kuwa mimi si mwovu;Wala hapana awezaye kuokoa na mkono wako?
8. Mikono yako imeniumba na kunifinyanga;Nawe utageuka na kuniangamiza?
9. Kumbuka, nakusihi ulivyonifinyanga kama vile udongo;Nawe, je! Utanirudisha uvumbini tena?
10. Je! Wewe hukunimimina kama maziwa,Na kunigandisha mfano wa jibini?