2 Tim. 4:6-12 Swahili Union Version (SUV)

6. Kwa maana, mimi sasa namiminwa, na wakati wa kufariki kwangu umefika.

7. Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda;

8. baada ya hayo nimewekewa taji ya haki, ambayo Bwana, mhukumu mwenye haki, atanipa siku ile; wala si mimi tu, bali na watu wote pia waliopenda kufunuliwa kwake.

9. Jitahidi kuja kwangu upesi.

10. Maana Dema aliniacha, akiupenda ulimwengu huu wa sasa, akasafiri kwenda Thesalonike; Kreske amekwenda Galatia; Tito amekwenda Dalmatia.

11. Luka peke yake yupo hapa pamoja nami. Umtwae Marko, umlete pamoja nawe, maana anifaa kwa utumishi.

12. Lakini Tikiko nalimpeleka Efeso.

2 Tim. 4