2. tukaokolewe na watu wasio haki, wabaya; maana si wote walio na imani.
3. Lakini Bwana ni mwaminifu, atakayewafanya imara na kuwalinda na yule mwovu.
4. Nasi tumemtumaini Bwana kwa mambo yenu, kwamba mnayafanya tulivyowaagiza, tena kwamba mtayafanya.
5. Bwana awaongoze mioyo yenu mkapate pendo la Mungu, na saburi ya Kristo.
6. Ndugu, twawaagiza katika jina la Bwana Yesu Kristo, jitengeni nafsi zenu na kila ndugu aendaye bila utaratibu, wala si kwa kufuata mapokeo mliyoyapokea kwetu.