18. Basi Wafilisti walikuwa wamekuja na kujitawanya bondeni mwa Warefai.
19. Basi Daudi akauliza kwa BWANA, akisema, Je! Nipande juu ya Wafilisti? Utawatia mkononi mwangu? Naye BWANA akamwambia Daudi, Panda; kwa kuwa hakika nitawatia Wafilisti mikononi mwako.
20. Basi Daudi akaja Baal-perasimu, naye Daudi akawapiga huko; akasema, BWANA amewafurikia adui zangu mbele yangu, kama mafuriko ya maji. Basi akapaita mahali pale Baal-perasimu.
21. Nao wakaziacha sanamu zao huko, na Daudi na watu wake wakaziondolea mbali.