2 Sam. 5:18-21 Swahili Union Version (SUV)

18. Basi Wafilisti walikuwa wamekuja na kujitawanya bondeni mwa Warefai.

19. Basi Daudi akauliza kwa BWANA, akisema, Je! Nipande juu ya Wafilisti? Utawatia mkononi mwangu? Naye BWANA akamwambia Daudi, Panda; kwa kuwa hakika nitawatia Wafilisti mikononi mwako.

20. Basi Daudi akaja Baal-perasimu, naye Daudi akawapiga huko; akasema, BWANA amewafurikia adui zangu mbele yangu, kama mafuriko ya maji. Basi akapaita mahali pale Baal-perasimu.

21. Nao wakaziacha sanamu zao huko, na Daudi na watu wake wakaziondolea mbali.

2 Sam. 5