8. Ndipo nchi ilipotikisika na kutetemeka,Misingi ya mbinguni ikasuka-sukaNa kutikisika, kwa sababu alikuwa na ghadhabu.
9. Kukapanda moshi kutoka puani mwake,Moto ukatoka kinywani mwake ukala;Makaa yakawashwa nao.
10. Aliziinamisha mbingu akashuka;Kukawa na giza kuu chini ya miguu yake.
11. Akapanda juu ya kerubi akaruka;Naam, alionekana juu ya mabawa ya upepo.
12. Akafanya giza hema zake za kumzunguka,Makusanyiko ya maji, mawingu makuu ya mbinguni.