2 Sam. 22:4-8 Swahili Union Version (SUV)

4. Nitamwita BWANA astahiliye kusifiwa;Hivyo nitaokoka na adui zangu.

5. Maana mawimbi ya mauti yalinizunguka,Mafuriko ya uovu yakanitia hofu.

6. Kamba za kuzimu zilinizunguka;Mitego ya mauti ikanikabili.

7. Katika shida yangu nalimwita BWANA,Naam, nikamlalamikia Mungu wangu;Naye akaisikia sauti yangu hekaluni mwake,Kilio changu kikaingia masikioni mwake.

8. Ndipo nchi ilipotikisika na kutetemeka,Misingi ya mbinguni ikasuka-sukaNa kutikisika, kwa sababu alikuwa na ghadhabu.

2 Sam. 22