4. Nitamwita BWANA astahiliye kusifiwa;Hivyo nitaokoka na adui zangu.
5. Maana mawimbi ya mauti yalinizunguka,Mafuriko ya uovu yakanitia hofu.
6. Kamba za kuzimu zilinizunguka;Mitego ya mauti ikanikabili.
7. Katika shida yangu nalimwita BWANA,Naam, nikamlalamikia Mungu wangu;Naye akaisikia sauti yangu hekaluni mwake,Kilio changu kikaingia masikioni mwake.
8. Ndipo nchi ilipotikisika na kutetemeka,Misingi ya mbinguni ikasuka-sukaNa kutikisika, kwa sababu alikuwa na ghadhabu.