1. Basi Daudi akamwambia BWANA maneno ya wimbo huu, siku ile BWANA alipomwokoa mikononi mwa adui zake zote, na mkononi mwa Sauli;
2. akasema,BWANA ndiye jabali langu, na ngome yangu, na mwokozi wangu,naam, wangu;
3. Mungu wa mwamba wangu, nitamwamini yeye;Ngao yangu, na pembe ya wokovu wangu, mnara wangu, namakimbilio yangu;Mwokozi wangu, waniokoa na jeuri.
4. Nitamwita BWANA astahiliye kusifiwa;Hivyo nitaokoka na adui zangu.
5. Maana mawimbi ya mauti yalinizunguka,Mafuriko ya uovu yakanitia hofu.
6. Kamba za kuzimu zilinizunguka;Mitego ya mauti ikanikabili.