1. Ahazi alikuwa na umri wa miaka ishirini alipoanza kutawala; akatawala katika Yerusalemu miaka kumi na sita; wala hakufanya yaliyo ya adili machoni pa BWANA, kama Daudi babaye;
2. bali akaziendea njia za wafalme wa Israeli, akawafanyizia mabaali sanamu za kusubu.