2 Nya. 27:3-5 Swahili Union Version (SUV)

3. Ndiye aliyelijenga lango la juu la nyumba ya BWANA, na juu ya ukuta wa Ofeli akajenga sana.

4. Tena akajenga miji katika milima ya Yuda, na mwituni akajenga ngome na minara.

5. Kisha akapigana na mfalme wa wana wa Amoni, akawashinda. Na wana wa Amoni wakampa mwaka ule ule talanta mia za fedha, na kori elfu kumi za ngano, na elfu kumi za shayiri. Hayo ndiyo waliyomtolea wana wa Amoni, mwaka wa pili pia, na mwaka wa tatu.

2 Nya. 27