19. Usikubali mashitaka juu ya mzee, ila kwa vinywa vya mashahidi wawili au watatu.
20. Wale wadumuo kutenda dhambi uwakemee mbele ya wote, ili na wengine waogope.
21. Nakuagiza mbele za Mungu, na mbele za Kristo Yesu, na mbele za malaika wateule, uyatende hayo pasipo kuhukumu kwa haraka; usifanye neno lo lote kwa upendeleo.
22. Usimwekee mtu mikono kwa haraka, wala usizishiriki dhambi za watu wengine. Ujilinde nafsi yako uwe safi.