1 Sam. 2:3-7 Swahili Union Version (SUV)

3. Msizidi kunena kwa kutakabari hivyo;Majivuno yasitoke vinywani mwenu;Kwa kuwa BWANA ni Mungu wa maarifa,Na matendo hupimwa na yeye kwa mizani.

4. Pinde zao mashujaa zimevunjika,Na hao waliojikwaa wamefungiwa nguvu.

5. Walioshiba wamejikodisha ili kupata chakula,Na hao waliokuwa na njaa wamepata raha.Naam, huyo aliyekua tasa amezaa watoto saba,Na yeye aliye na wana wengi amedhoofika.

6. BWANA huua, naye hufanya kuwa hai;Hushusha hata kuzimu, tena huleta juu.

7. BWANA hufukarisha mtu, naye hutajirisha;Hushusha chini, tena huinua juu.

1 Sam. 2