1 Kor. 15:55-58 Swahili Union Version (SUV)

55. Ku wapi, Ewe mauti, kushinda kwako? U wapi, Ewe mauti, uchungu wako?

56. Uchungu wa mauti ni dhambi, na nguvu za dhambi ni torati.

57. Lakini Mungu na ashukuriwe atupaye kushinda kwa Bwana wetu Yesu Kristo.

58. Basi, ndugu zangu wapendwa, mwimarike, msitikisike, mkazidi sana kutenda kazi ya Bwana sikuzote, kwa kuwa mwajua ya kwamba taabu yenu siyo bure katika Bwana.

1 Kor. 15