32. Ikiwa, kwa jinsi ya kibinadamu, nalipigana na hayawani wakali kule Efeso, nina faida gani? Wasipofufuliwa wafu, na tule, na tunywe, maana kesho tutakufa.
33. Msidanganyike; Mazungumzo mabaya huharibu tabia njema.
34. Tumieni akili kama ipasavyo, wala msitende dhambi; kwa maana wengine hawamjui Mungu. Ninanena hayo niwafedheheshe.
35. Lakini labda mtu atasema, Wafufuliwaje wafu? Nao huja kwa mwili gani?
36. Ewe mpumbavu! Uipandayo haihuiki, isipokufa;
37. nayo uipandayo, huupandi mwili ule utakaokuwa, ila chembe tupu, ikiwa ni ya ngano au nyingineyo;