1 Fal. 7:42-45 Swahili Union Version (SUV)

42. na makomamanga mia nne ya zile nyavu mbili; safu mbili za makomamanga kwa kila wavu, kuzifunika hizo vimbe mbili za taji zilizokuwa juu ya nguzo;

43. na yale matako kumi, na birika kumi juu ya matako;

44. na ile bahari moja, na ng’ombe kumi na wawili chini ya ile bahari;

45. na masufuria, na majembe, na mabakuli; hata vyombo hivyo vyote, Huramu alivyomfanyia mfalme Sulemani, katika nyumba ya BWANA, vyote vilikuwa vya shaba iliyosuguliwa.

1 Fal. 7